DJ NYASI24.COM

DJ NYASI24.COM

Saturday, September 28, 2013

ANGALIA PICHA ZIKIMWONYESHA MSANII DIAMOND AKIWA NDANI YA STUDIO KUBWA DUNIANI ZA COKE

Mkali wa Ngololo 'Diamond Platnumz' ambaye anahusika kwenye matangazo ya kampuni ya Cocacola ametupia picha akiwa kwenye Coke Studio za Africa kupitia account yake ya Instragram na haya ndiyo aliyo yaandika.

Thursday, August 22, 2013

NEW SONG NAIJA / PSquare – Makossa Fiesta

P-square
Brand New Music from the twins,they are going on tour  by the way.

RWANDA NA UGANDA WAJITOA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Chama cha Wasafirishaji wa Mafuta Tanzania (Tatoa), kimesema Rwanda na Uganda zitajitoa kutumia Bandari ya Dar es Salaam kuanzia Septemba Mosi, mwaka huu.

Katibu Mtendaji wa Tatoa, Zacharia Hanspope aliwaambia waandishi wa habari jana baada ya kukutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuwa nchi hizo zinajitoa kutokana na matatizo mbalimbali ambayo kwa muda mrefu zimekuwa zikiyalalamikia lakini Serikali haikuchukua hatua.

 Hanspope alisema ushuru wa barabara na ushuru wa forodha ni baadhi ya vikwazo ambavyo vimekuwa vikilalamikiwa kwa muda mrefu na wafanyabiashara mbalimbali wa nchi hizo.


“Serikali ipunguze gharama za ushuru wa barabara na ushuru wa forodha ili kuwa na ushindani sawa na bandari nyingine na hivyo kuzivutia kutumia Bandari ya Dar es Salaam,” alisema Hanspope.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Omary Chambo alikataa kuzungumzia lolote kuhusu suala hilo akisema halina mantiki yoyote kwake.... “Hivi hilo jambo unaloniuliza lina sense (mantiki) yoyote? Mie siwezi kujibu lolote nenda ukamuulize mwenyewe (Hanspope) maana wakati akisema mimi sikuwepo.”

Alisema kujitoa kwa Rwanda na Uganda kuitumia Bandari ya Dar es Salaam hakutakiathiri chama hicho tu, bali uchumi wa taifa kwa ujumla.

Hayo yanatokea wakati Rwanda ikiendeleza vita yake ya maneno na Tanzania na mfululizo wa matukio ya kuitenga Tanzania kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki. Viongozi wa Kenya, Rwanda na Uganda walikutana Juni 25, mwaka huu mjini Entebbe, Uganda na kukubaliana kuongeza uhusiano wa kibiashara baina yao.

Kamati ya Bajeti:

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Andrew Chenge alisema katika kikao kijacho cha Bunge, kamati hiyo itaibana Serikali kuhusu mikakati inayofanywa kukabiliana na ushindani wa kibiashara katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Alisema sababu ya Rwanda na Uganda kujitoa kutumia Bandari ya Dar es Salaam ni vikwazo katika barabara ikiwamo mizani mingi ya kupimia mizigo.

“Mizani ni mingi pia kuna usumbufu katika kupima mizigo yao na kwamba hali hiyo inawaletea usumbufu wafanyabiashara wengi,” alisema.

Alisema vitendo vya askari wa usalama barabarani kudai rushwa pia ni miongoni mwa vikwazo pamoja na urasimu mkubwa katika utoaji wa mizigo bandarini ikilinganishwa na bandari nyingine.

“Ni lazima tujifunze kwa majirani zetu Msumbiji, upanuzi wa haraka wa Bandari ya Beira umekuwa kikwazo kwetu, kampuni nyingi zimeanza kuitumia bandari hiyo,” alisema.

Chenge alikitaka chama hicho kuiandikia kamati hiyo mapendekezo yake ikiwa ni hatua ya kunusuru uchumi wa nchi ili waweze kuijadili bungeni.

Umoja wa nchi tatu:

Marais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Paul Kagame wa Rwanda na mwenyeji wao Yoweri Museveni walikutana mjini Kampala, Uganda na kuamua kuitumia Bandari ya Mombasa kwa shughuli zao.

Waliahidi kuimarisha ufanisi katika huduma za Bandari ya Mombasa ili kuhakikisha bidhaa zinafika mapema Uganda na Rwanda.

Pia walikubaliana kujenga reli mpya ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa kutoka Mombasa kwenda Kenya na Uganda.

Viongozi hao walikubaliana pia kushirikiana katika sekta ya nishati hasa ikizingatiwa kuwa Uganda imegundua mafuta.

Nchi hizo tatu ambazo zimeruhusu kwa raia wao kusafiri kwa vitambulisho pale wanapotembelea nchi tatu miongoni mwao, zitakutana tena Kenya mwezi huu.

Source:Mwananchi

Friday, July 12, 2013

[Offical Music Video ]MALAIKA - Dogo scope & Tenya Brown

Kama kweli Bhakhresa atafanya hivi, wafuasi wake wataongezeka



996796_379903418798881_736826428_n
Hili ni dish la AzamTV ambayo inazungumziwa
 
Taarifa zilizoenea chinichini kwa sasa ni kwamba kuna kitu kingine kipya kutoka kwa kampuni ya Azam ambayo ni maarufu kwa kutengeneza bidhaa za vyakula, usafirishaji abiria kwa njia ya boti na hata michezo pia kupitia Azam FC ambapo kampuni hii inadaiwa kukaribia kutambulisha king’amuzi ambacho kitakua na uwezo wa kuonyesha Tv channel mbalimbali zikiwemo za Tanzania pia. Taarifa hizo za chinichini zimezidi kuamplfy kwamba gharama yake ya malipo ya kila mwezi itakuwa ndogo zaidi ya ving’amuzi vyote kwa Tanzania na watumiaji kwa kila mwezi watatakiwa k
Huu ni uwanja wanaoumiliki Azam FC Chamazi Mbagala Dar es salaam.
ulipia pesa za kitanzania Shilingi elfu mbili tu…… hata hivyo NYASI.COM. inazidi kufatilia kupata info zaidi

Unaambiwa hii ndio video mpya ya Mwanamke akimpiga mume wake hadharani Kenya

.
Ni ngumu kumuona mwanaume akitokwa machozi kama hivi…. hii imetokana na mke wake kumpiga makofi hadharani kwenye mji wa Meru nchini Kenya ambapo Mwanamke huyo alikua anadai jamaa kamkana, japo anasisitiza kwamba ni mume wake na ndio baba wa watoto mapacha akiwemo mmoja alienae mgongoni, Mwanaume alikataa kabisa na kusema hata watoto sio wake.
Taarifa ambayo imerushwa na KTN Kenya, ni kwamba alichotaka Mwanamke ni Mwanaume huyo akubali tu kwamba ni mume wake na pia ndio baba watoto wa mapacha hao… lakini Mwanaume aliapa kabisa kwamba hausiki kwenye upande wowote, hicho ndio kilichompa hasira Mwanamke na kuanza kumpiga na baadae pia kusaidiwa kupiga na Mwanamke aliekua nae.
Kenya imekua kwenye mfululizo wa kesi za Wanawake kupiga waume zao nyumbani na hadharani pale wanapokosana ambapo February 2012 Umoja wa Wanaume Kenya ulitangaza kususia kula majumbani kwa wiki moja na kununua chakula hotelini mpaka Serikali itakapoingilia usawa wa Wanaume na kuhakikisha tabia ya Wanawake kupiga Waume zao inamalizwa.

.

Thursday, July 11, 2013

hashim shedrack - pamsalaba.mp3 @Hulkshare:

 hashim shedrack - pamsalaba.mp3 @Hulkshare:

MAMA MZAZI WA PROFESA J AFARIKI DUNIA BAADA YA KUNGONGWA NA GARI USIKU WA LEO HUKO MBEZI JUU, DAR ES SALAAM

Profesa J akiwa na mama yake mzazi Bi Rosemary Majanjara Haule enzi za uhai wake.  Picha hii ilipigwa April 4, 2008 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam  wakati wa sherehe ya uzinduzi wa albamu mpya ya Profesa J ya 'Aluta Continua'


HABARI ZILIZOPOKEWA USIKU HUU NI KWAMBA MAMA YAKE MZAZI MSANII MAARUFU WA MUZIKI NCHINI, JOSEPH HAULE A.KA. 'PROFESA J' AMEFARIKI DUNIA USIKU HUU BAADA YA KUGONGWA NA GARI  MAENEO YA MBEZI JUU, JIJINI DAR ES SALAAM, ALIKOKUWA ANAISHI NA MWANAE.

HABARI ZINASEMA MAREHEMU, BI. ROSEMARY MAJANJARA HAULE, ALIGONGWA NA GARI AKIWA ANAVUKA BARABARA KUELEKEA DUKANI KIASI CHA SAA MBILI USIKU, NA KWAMBA BAADA YA KUGONGWA WASAMARIA WEMA WALIMKIBIZA HOSPITALINI TUMBI KWA KUTUMIA BAJAJI AMBAKO ALIFARIKI DUNIA. TAARIFA ZA AWALI HAZIJATAJA AINA YA GARI NA KAMA BAADA YA AJALI HIYO LILISIMAMA AU LA.

PROFESA J AMETHIBITISHA  HILO MUDA MFUPI ULIOPITA, NA KUSEMA INAMUIA VIGUMU KUAMINI IMETOKEA KWANI ANASEMA MAREHEMU MNAMO SAA MBILI HIVI ALIMPIGIA SIMU NA KUMWELEZA KUWA AMEPATA AJALI NA KWAMBA WAKATI HUO YUKO KITUO CHA POLISI, BILA SHAKA KUPATA FOMU YA PF 3 YA KUMUWEZESHA KWENDA KUTIBIWA HOSPITALI.

"MAMA ALINIAMBIA MWANANGU NIMEGONGWA NA GARI....NJOO NIKO POLISI NAANDIKISHA....MWANANGU NAKUFA....ALINIAMBIA MAMA NA MARA SIMU IKAKATIKA. KILA NILIPOJARIBU KUPIGA IKAWA HAIPATIKANI..." ALISEMA PROFESA J KWA UCHUNGU.

ANASEMA WAKATI ANAPIGIWA SIMU NA MAMA YAKE YEYE ALIKUWA KATIKA MGAHAWA WA NYUMBANI LOUNGE, NAMANGA, DAR ES SALAAM, ALIKOKUWA KATIKA KIKAO NA LADY JAY DEE NA MUMEWE GADNA G. HABASH, AMBAO BAADA YA TAARIFA HIYO WALIMSINDIKIZA HADI HOSPITALI YA TUMBI.

"TULIPOFIKA HOSPITALI SIKUAMINI KUONA BADALA YA KUPELEKWA WODINI AMBAKO NILIDHANI MAMA ATAKUWA AMELAZWA NIKAPELEKWA CHUMBA CHA MAITI AMBAKO NILIMKUTA MAMA AKIWA MAREHEMU", ALISEMA PROFESA J KWA MAJONZI.

GLOBU YA JAMII INATOA MKONO WA POLE KWA PROFESA J KWA MSIBA HUU MZITO NA WA KUSIKITISHA. TUNAMWOMBA MOLA AMPE NGUVU YEYE NA FAMILIA YAKE KATIKA WAKATI HUU MGUMU. 

TUTAENDELEA KUWAPASHA KINACHOJIRI KADRI HABARI  ZAIDI ZITAPOPATIKANA. KWA SASA PROFESA J NA WADAU WENGINE WAKO NYUMBANI KWAKE MBEZI JUU.

Tuesday, July 2, 2013

MMILIKI WA FACEBOOK AKISHEREKEA KUPITISHWA KWA NDOA YA JINSIA MOJA

Mmiliki wa mtandao wa kijamii Facebook CEO Mark Zuckerberg amejiunga na wafanyakazi wa kampuni yake waliozidi 700 katika matembezi ya kusherekea maamuzi ya mahakama kuhusu haki za ndoa ya jinsia moja. Matembezi haya yamefanyika mitaa ya San Francisco Jumapili Asubuh. Kwa mujibu wa Wall Street Journal asilimia 15 ya wafanyakazi wa facebook.

Sheria hio inayo sherekewa Imeruhusu wanandoa wa jinsia moja kumiliki leseni ya ndoa ndani ya siku 30 baada ya kuoana. 

Thursday, June 27, 2013

Mzee Mandela afanyiwa maombi maalum

JOH'BURG-AFRIKA KUSINI, Askofu mkuu wa kanisa la kianglikana mjini Cape Town, Afrika Kusini, Thabo Makgoba, amejitolea kufanya maombi kwa niaba ya rais mstaafu Nelson Mandela ambaye anaugua sana hospitalini.
Kasisi huyo anamuombea Mandela aweze kupata nafuu na amewataka wananchi kumshukuru kwa yote aliyowafanyia.


Jamaa za Nelson Mandela wamekutana nyumbani kwake huko Kunu, huku hali yake ya afya ikizidi kudorora hospitalini, Pretoria.

Afya ya Bwana Mandela ilikuwa mbaya zaidi Jumapili.
Maombi hayo yalitolewa baada ya Askofuu huyo kumtembelea Mandela hospitalini ambako kiongozi huiyo wa zamani amekuwa akilazwa kwa wiki mbili na nusu zilizopita baada ya kuugua mapafu.

Vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa wajukuu wa rais huyo wa zamani wa Afrika kusini wanakutana nyumbani kwake kijijini katika mkoa wa Eastern Cape province, ambako viongozi wa kitamaduni wamealikwa.

Halikopta ya jeshi kadhalika zilionekana zikipaa karibu nyumbani kwa mandela. Afisi ya Rais jacob Zuma ilitangaza jumapili kuwa hali ya mzee

Wednesday, June 26, 2013

JE? UNA YAKUMBUKA YALIOKUWA YAMESEMWA NA Mh WAZIRI tembelea BLOG HII

PINDA TENA

WAANDISHI WA HABARI WAWEKA KAMBI KARIBU NA HOSPITALI ALIKOLAZWA NELSON MANDELA



Rais mstaafu wa Afrika Kusini NELSON MANDERA bado anahali mbaya ingawa bado madaktari yana pigania uhai wake baada ya afya yake kuzorota mwishoni mwa wiki......Richa ya hivyo imeonekana kuwa watu wamepoteza matumaini na kujiandaa kwa loloye ambolo linaweza kutokea mda wowote.
Waandishi na vyombo vya habari viko karibu kabisa na hospitali hiyo kusubiri lolote litakalotokea .

Tuesday, June 25, 2013

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Kenya Ibra Da Hustler akiwa katika pozi
WAKATI kesho dunia inaadhimisha siku ya matuizi ya dawa za kulevya Rapper Ibra Da Hustler amefunguka kuwa sasa anampango wa kubadilisha maisha yake kwa uamuzi aliouchukuwa wa kuachana na matumizi ya dawa aina ya Herion na Crack Cocaine.

Da Hustler ameamua kuachana na matumizi hayo ya dawa za kulevya baada ya kuona kuwa ni uharibifu wa pesa pili kitendo hicho ni kukaribisha dharau kwenye maisha yake huku akihatarisha maisha, Rapper huyo ambaye kwa sasa ana takribani siku nne hajagusa toka amejiunga na taasisi amejifunza kuvumilia na matumaini yake ni kuachana kabisa na matumizi hayo ya dawa za kulevya.

Akizungumza na habarimpya.com alisema kwamba mwanamke ndiye aliyemshawishi mpaka akiingiza katika matumizi ya dawa ya kulevya. “Kuna binti alinishawis kutumia dawa na ndio nikajikuta nimeingia katika mkumbo huu najuta kumfahamu nakubaini kuwa hataki maendeleo yangu kabisa nanimejifunza kutoka kwake, sasa nikimwambia mtu usiguse dawa ataamini kwani najua kitu gani atapata kwenye maisha yake”alisema Dar Hustler.

“Nimeacha Kabisa madawa nina siku nne sijagusa toka nimejiunga na hii taasisi ya kuwaelimisha watu wanaohitaji kuachana na dawa za kulevya, nimejifunza kuvumilia arosto na matumaini yangu ni kuacha kabisa dawa kwani yameharibu maisha yangu kabisa".

Alisema kwamba matumizi ya dawa za kulevya ni uharibifu wa pesa nyingi na kwamba amekaribisha dharau kwenye maisha yake.

Rapper huyo alisema endapo atafanikiwa kuachana na matumizi ya dawa za kulevya atarudi katika kazi yake ya muziki, kwani anaamini ndiyo kazi pekee anayoiweza na mashabiki wake watakuwa wamemis kazi zake."Kundi la wanamuziki wa Nako 2 Nako na Weusi wananipa ushirikiano mzuri sana, wote wamefurahi kusikia nimeanza kuachana na dawa za kulevya".

akizungumzia wimbo wake wa sababu ni wewe, anasema kwamba,"niliimba mambo yote yaliyonitokea tangu nilipoanza kutumia dawa ya kulevya na jinsi yalivyo niharibia maisha yangu, matumaini yangu kwa vijana wanaotumia dawa watajifunza kutoka kwangu kuhusu madhara ya dawa za kulevya. 

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Kenya Ibra Da Hustler akiwa katika pozi
WAKATI kesho dunia inaadhimisha siku ya matuizi ya dawa za kulevya Rapper Ibra Da Hustler amefunguka kuwa sasa anampango wa kubadilisha maisha yake kwa uamuzi aliouchukuwa wa kuachana na matumizi ya dawa aina ya Herion na Crack Cocaine.

Da Hustler ameamua kuachana na matumizi hayo ya dawa za kulevya baada ya kuona kuwa ni uharibifu wa pesa pili kitendo hicho ni kukaribisha dharau kwenye maisha yake huku akihatarisha maisha, Rapper huyo ambaye kwa sasa ana takribani siku nne hajagusa toka amejiunga na taasisi amejifunza kuvumilia na matumaini yake ni kuachana kabisa na matumizi hayo ya dawa za kulevya.

Akizungumza na habarimpya.com alisema kwamba mwanamke ndiye aliyemshawishi mpaka akiingiza katika matumizi ya dawa ya kulevya. “Kuna binti alinishawis kutumia dawa na ndio nikajikuta nimeingia katika mkumbo huu najuta kumfahamu nakubaini kuwa hataki maendeleo yangu kabisa nanimejifunza kutoka kwake, sasa nikimwambia mtu usiguse dawa ataamini kwani najua kitu gani atapata kwenye maisha yake”alisema Dar Hustler.

“Nimeacha Kabisa madawa nina siku nne sijagusa toka nimejiunga na hii taasisi ya kuwaelimisha watu wanaohitaji kuachana na dawa za kulevya, nimejifunza kuvumilia arosto na matumaini yangu ni kuacha kabisa dawa kwani yameharibu maisha yangu kabisa".

Alisema kwamba matumizi ya dawa za kulevya ni uharibifu wa pesa nyingi na kwamba amekaribisha dharau kwenye maisha yake.

Rapper huyo alisema endapo atafanikiwa kuachana na matumizi ya dawa za kulevya atarudi katika kazi yake ya muziki, kwani anaamini ndiyo kazi pekee anayoiweza na mashabiki wake watakuwa wamemis kazi zake."Kundi la wanamuziki wa Nako 2 Nako na Weusi wananipa ushirikiano mzuri sana, wote wamefurahi kusikia nimeanza kuachana na dawa za kulevya".

akizungumzia wimbo wake wa sababu ni wewe, anasema kwamba,"niliimba mambo yote yaliyonitokea tangu nilipoanza kutumia dawa ya kulevya na jinsi yalivyo niharibia maisha yangu, matumaini yangu kwa vijana wanaotumia dawa watajifunza kutoka kwangu kuhusu madhara ya dawa za kulevya. 

Monday, June 24, 2013

THE REASON OF US PRESIDENT BARRACK OBAMA TO SKIP KENYA


President Barack Obama
NAIROBI, KENYA: US President Barack Obama has explained his itinerary did not include Kenya because the International Criminals Court (ICC) had indicted President Uhuru Kenyatta and his Deputy William Ruto.
What is more, Obama also appeared to downgrade Kenya’s place in the region by singling out Tanzania as America’s key ally in the East Africa region.
In a Press briefing on Obama’s upcoming trip to Senegal, South Africa and Tanzania via conference call, US Deputy National Security Advisor Ben Rhodes said it was not the best time for the US President to visit Kenya.
“Given the fact that Kenya is in the aftermath of their election and the new government has come into place and is going to be reviewing these issues with the ICC and the international community, it just wasn’t the best time for the President to travel to Kenya at this point,” said Mr Rhodes.
He said though President Obama had deep personal and familial connections to Kenya, the US, as a country, had a commitment to accountability and justice as a baseline principle.
Sovereign right
“He has visited there in the past as a private citizen and as a senator, and the Kenyan people just held a very special place in the President’s heart,” he said.
The official said US fully respected the sovereign right of the Kenyan people to choose their leaders and would certainly be focused on working with the new Kenyan government under President Kenyatta.
He, however, indicated that Tanzania was currently an important partner for the US in the region.
“ Tanzania is one of the significant US foreign assistance partners as well as a strong democracy, so we felt like Tanzania was an important stop in East Africa,” Rhodes said. He, however, clarified that there were no plans to have the US President’s step-grandmother Sarah meet him in Tanzania.

“I would note that his sister Auma Obama was with us in Berlin and was able to attend the speech and the State dinner, and that’s obviously a very close family member of the President’s from that side of his family,” said Rhodes.
The president, along with his wife, Michelle, and daughters Malia and Sasha, is scheduled to depart Washington on Wednesday morning.
In February, a month before the elections, US Assistant Secretary of State for African Affairs Johnnie Carson warned the country that the choice of President ‘would have global consequences’.
Warned
Mr Carson said in as far as the elections was a Kenyan affair; its outcome would have implications given that the country was bound to interact with the international community.
“US does not have a candidate in the elections, however, choices have consequences. We live in an interconnected world and people should be thoughtful about the impact their choices have on their nation, economy region,” he said.
Since he was sworn-in President Kenyatta has visited a number of countries, among them the United Kingdom, which had initially also warned of having only ‘essential contacts’.
“It is well known the position of my government and others is that we don’t get in contact with the ICC indictees unless it is essential,” said Christian Turner, the United Kingdom envoy to Kenya. Ms Jendayi Frazer, a former United States Assistant Secretary of State for African Affairs two months ago warned US against playing a dangerous game for their delayed endorsement of Kenyatta.
“If the US, the UK and the Europeans don’t want to deal with Uhuru Kenyatta, he has other options,” she said in an interview with American TV channel PBS.
“The West risked losing its strategic influence in the region,” she warned.
By Jacob Ngetich, The Standard

Friday, June 21, 2013

PICHA YA MBUNGE MOSES MACHALLIA AKIWA HOSPITALI YA GENERAL DODOMA


Mbunge Moses Machallia NCCR (Kasulu Mjini)
Katika picha ni mbunge machallia wa NCCR Kasulu mjini akiwa amelazwa wodini maalum katika hospitali ya General dodoma baada ya kupigwa na watu wasiojulikana usiku wa jana na kumjeruhi.Tukio hili lilitokea katika eneo la area E mjini dodoma wakati akitoka kuhudhuria kikao cha bunge la bajeti.

MWANAFUNZI UDSM APIGWA RISASI TUMBONI





Taarifa zilizotufikia katika chumba cha habari zinaeleza kuwa wanafunzi wanne wa chuo kikuu cha Dar es salaam maarufu kwa jina la Chuo cha Mlimani wamevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo maeneo ya Yombo chuoni hapo.
Wanafunzi hao wanaosemekana kuwa ni wa mwaka wa nne na wa mwisho wa masomo walikuwa wanajisomea na kuandaa “Disertation” zao na kujikuta wakivamiwa na watu wanne na kuamuriwa watoe komputa zao na pochi za fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo, wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha,  na majambazi kuanza safari yao.

Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.

Chanzo kimeendelea kusema kuwa wanafunzi wa Chuo hicho waliwasiliana na uongozi ili kupata gari ili wamkimbize mwenzao Hospitalini, lakini ilipita takribani nusu saa hakuna majibu na ndipo walipoamua kujikusanya na kuamua kuwafuata viongozi. Kwa sasa mwanafunzi huyo amekimbizwa Hospitalini kupata matibabu zaidi na mpaka sasa hakuna taarifa yoyote iliyotoka, ingawa FULLSHANGWE inajitahidi kufuatilia suala hilo ili kupta taarifa zaidi na picha za tukio hilo.

Tukio hilo limelaaniwa vikali na UMMA wa chuo kikuu cha Dar es salaam na kuitaka serikali kufuatiliwa na kudhibiti vitendo hivyo vya kikatili chuoni hapo. Endelea kufuatilia katika mtandao huu amboa umefunga safari ya kuelekea Chuo kikuu cha Mlimani kuangalia nini kinaendelea.

Mbali na tukio hilo, pia kumekuwepo na wizi wa hadharani katika shule za Chuo hicho ambapo hivi karibuni wanafunzi wamekuwa wakiporwa komputa zao mchana kweupe maeneo ya Mikocheni wakitoke shule kuu ya uandishi wa Habari na Mawasilinao ya Umma (SJMC).

Suala hizi limepoteza amani kwa wanafunzi na kuwafanya washindwe kusoma kwa amani

WEMA NA KAJALA KIMENUKA SASA NI PAKA NA CHUI HAZIIVI TENA


KIMENUKA! Utabiri wa wengi kuwa ushosti wa waigizaji masistaduu wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu na Kajala Masanja kutumbukia nyongo unadaiwa kutimia na sasa wametibuana, Ijumaa limenyetishiwa.


Wema katika pozi na Kajala.
Habari za ndani kutoka kwa mtu wa karibu (jina linahifadhiwa), mwanzoni baada ya Wema kumlipia Kajala faini ya Sh. milioni 13 na kumnusuru kutokwenda Segerea a.k.a Segedansi, wawili hao walikuwa marafiki kama pete na kidole.
SIKU KAMA HIZI
“Walishinda wote, walilala wote, walikwenda klabu wote yaani Kajala alikuwa anamnyenyekea ‘madam’ Wema kwa kumuepusha na kifungo cha miaka 7 jela,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Kuna wakati hapa katikati Kajala alikuwa kama katibu muhtasi wa madam, si unajua lazima atumikie fedha za watu?
“Kabla hajaenda Mwanza kwa ajili ya mapumziko kwa bibi zake, nilimsikia Kajala akilalama kuwa madam aliamka siku moja akawa amemchunia, unaambiwa hata salamu ikawa hakuna.

Wema akimlisha keki Kajala wakati wa sherehe ya kumkaribisha uraiani.

TATIZO NI WAPAMBE
“Hapo ndiyo maneno ya pembeni yakaanza kwa sababu mbali na Kajala, Wema pia ana wapambe wengine na mbali na Wema, Kajala naye ana kampani. Kwa hiyo sosi ya manenomaneno ni hizo kampani zao.
“Ipo siku kabisa Wema alimlalamikia Kajala hadharani kuwa amekuwa akimsema vibaya kwa watu.
“Yale maneno yalimuuma sana Kajala, ikabidi arudi nyumbani kwao lakini akawa anaogopa kumwambia mama yake kuwa ametibuana na Wema hadi alipotimkia Mwanza.


KUMBE ALIMKOSESHA DILI?
“Lakini kabla ya hii ishu ya kulaumiana, kipindi cha nyuma kidogo Kajala alipata dili la kwenda kurekodi filamu nchini China na mastaa wengine lakini ikadaiwa kuwa Wema alichomoa hivyo mwigizaji huyo hakwenda pamoja na kwamba alishapewa baraka zote na baba yake.
“Unaambiwa alikuwa amekamilisha taratibu zote za kwenda China, hadi tiketi alikuwa ameshakata lakini suala hilo lilipotua kwa Wema, ilidaiwa kuwa alikataa kumruhusu.


TATIZO MILIONI 13?
“Mimi nakwambia zile milioni 13 zinamkosesha raha Kajala hadi unamuona kabisa kwamba ana stress (msongo wa mawazo).
“Wewe fikiria, kazi inayomwingizia mkwanja ni filamu, sasa unaambiwa inadaiwa kuwa madam hataki acheze filamu za watu wengine, sasa ataishije jamani?


SASA NI KUNUNIANA KWA KWENDA MBELE
“Mimi nakwambia ndiyo maana ameamua kwenda kupumzika Mwanza baada ya kuwa wananuniana kwa kwenda mbele.”
Baada ya kupata habari hizo, Ijumaa lilimtafuta Wema kwa njia ya kilongalonga chake cha kiganjani ili kupata undani wa sakata hilo lakini hakupatikana hewani.


NYUMBANI KWA WEMA
Baadaye mwanahabari wetu alisaga lami hadi kwa staa huyo Kijitonyama, Dar, alipogonga geti alitoka mlinzi aliyedai kuwa ‘malkia’ alikuwa ndani amelala na hakuhitaji usumbufu pamoja na kwamba ilikuwa saa 6:30 mchana.


MENEJA WAKE ANASEMAJE?
Hata hivyo, Ijumaa lilibisha hodi ofisini kwa Wema, Mwananyamala-Komakoma ili kuzungumza na meneja wake, Martin Kadinda ambaye alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli Kajala yupo Mwanza, aliomba ruhusa ya kwenda kupumzika tukampa. Hayo mengine ya kutibuana na madam siwezi kuyasemea kwa sababu yapo nje ya uwezo wangu.
“Lingekuwa ni suala la kazi hapo sawa lakini ni vizuri ukazungumza na mkurugenzi mwenyewe (Wema) lakini sidhani kama ataweza kuzungumza kwa sababu alikuwa anaumwa, amezidiwa na kupelekwa hospitali.”


WEMA ANAUMWA NINI?
Alipoulizwa Wema anaumwa nini, Kadinda alifunguka: “Sijajua lakini ugonjwa ni siri kati ya mhusika na daktari, cha msingi wewe ujue tu anaumwa.”


HUYU HAPA KAJALA
Baada ya kupita kote huko kusaka undani wa sakata hilo, Ijumaa lilimgeukia Kajala kwa njia ya simu ya mkononi akiwa jijini Mwanza na kumuuliza kulikoni kutibuana na Wema.
Huku sauti ikiwa chini, Kajala alisema: “Ni kweli kuna hali ambayo hata mimi mwenyewe nashindwa kuelewa lakini siwezi kuzungumzia kwa leo nikiamini yatapita.”


Gazeti la Ijumaa

WAPIGA NONDO MJINI IRINGA WAKITHIRI OPARETION KALI YA KUWAKAMATA YAANZA AKAMATWA MMOJA NA KUSHUSHIWA KIPONDO KIKALI NA WANANCHI WENYE HASIRA.STORI NZIMA HII HAPA



Huyu ni miongoni mwa wapiga nondo katika mkoa wa IRINGA akipokea kichapo kikali huku akiwa chini ya ulinzi mkali kuelekea kituo cha polisi, jamaa huyu anayefahamika kwa jina la MASTER, Amekamatwa mara tuu baada ya mwenzake kukamatwa leo hii asubuhi akidaiwa naye kuhusika na uharifu huo. hii imetokea mara tuu baada ya matukio ya namna hiyo kulipotiwa mara kwa mara siku za karibuni
                      
 Baadhi ya wananchi mkoani IRINGA wakiwa na hasira na kutembeza kichapo kwa muharifu huyo kwakua wamechoshwa na matukio hayo yaliyokisiri sana mkoani Iringa


 
        
   Mtuhumiwa akiwa katika hali ngumu maana wananchi wana hasira sana na watu wa namna hiyo kuwafanyia unyama kwa kuwapiga nondo na kuwapora mali zao

 Wananchi wakiwa hawaogopi askari na wakiendelea kumpa kichapo mharifu huyo uku safari ya kuelekea kituoni ikiendelea


      
 Watu wakiwa wengi kusaka na kuwakabidhi watuhumiwa hao mikononi mwa polisi

   
Wananchi wakishangaa kilichojili leo mjini Iringa

Snura Majanga {Official Music Video

Sunday, June 16, 2013

KATIKA HARAKATI ZA KUTAFUTA UKOMBOZI WA NCHI



                                               DJ NYASI ON MIXING
MIMI PIA NI MWANA HARAKATI

Blog Archive

DENIS LUKOSI - MUNGU KAFANYA YAKE